Monday, 6 April 2015

KUDUMU KATIKA KUMWAMINI MUNGU WAKATI UNA TATIZO LA KIFEDHA




KUDUMU KATIKA KUMWAMINI MUNGU WAKATI UNA TATIZO LA KIFEDHA.......

  Nawasalimu katika jina la Bwana Yesu kristo..Ni wasaa mzuri tena napata kibali mbele zake na kujumuika nanyi katika kutangaza neno lake kama tulivyoamriwa tunasoma kitabu cha Mathayo 28:20...''na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaarumu ninyi''...Katika masomo yaliyopita nina imani kwa jina la Yesu kristo umeongeza kitu katika ufahamu wako. Kuna  mahala Mungu amekukusudia kufika katika jina la Yesu kristo..Barikiwa wewe ambaye umeamua kuchukua uamuzi mzuri wa kujifunza pamoja nami...
Ndugu mpendwa katika Bwana tutajifunza somo lenye kichwa cha habari.."KUDUMU KATIKA KUMWAMINI MUNGU WAKATI UNA TATIZO LA KIFEDHA..'' Katika maisha yetu ya kila siku fedha imechukua nafasi kubwa sana....kila kitu tukifanyacho kinahitaji fedha..Si Elimu,Ujenzi,Injili,n.k. Fedha hizi pia mbali ya kuwa muhimu pia ni changamoto kuzipata na katika familia fulani fulani zimekuwa ni kama ndoto..Hebu ndugu mpendwa tujiulize swali hili lenye changamoto ya kibinadamu...Mahusiano yako na Mungu yapoje wakati una tatizo la kifedha? Je? unadumu katika yeye au unamkosea na kutenda dhambi...Ukiwa unatafakari nafasi yako katika jibu hili..ningependa tushiriki kwa pamoja kusoma hadithi ya mjane mmoja katika Biblia katika kitabu kile cha 2 Wafalme 4:1-7....

''Basi,mwanamke mmoja miongoni mwa wake za wana wa manabii alimlilia Elisha,akasema,Mtumishi wako mume wangu amekufa; nawe unajua ya kuwa mtumishi wako alikuwa mcha BWANA; na aliyemwia amekuja ili ajitwalie wana wangu wawili kuwa watumwa. Elisha akamwambia,Nikufanyie nini? Niambie; una kitu gani nyumbani? Akasema, Mimi mjakazi wako sina kitu nyumbani,ila chupa ya mafuta. Akasema,Nenda,ukatake vyombo huko nje kwa jirani zako wote,vyombo vitupu;wala usitake vichache. Kisha uingie ndani,ukajifungie mlango wewe na wanao,ikavimiminie mafuta vyombo vile vyote; navyo vilivyojaa uvitenge. Basi akamwacha,akajifungia mlango yeye na wanawe; hao wakamletea vile vyombo,na yeye akamimina. Ikawa,vilipokwisha kujaa vile vyombo,akamwambia mwanawe,Niletee tena chombo. Akamwambia,Hakuna tena chombo. Mafuta yakakoma. Ndipo akaja akamwambia yule mtu wa Mungu. Naye akasema,Enenda ukayauze mafuta haya,uilipe deni yako;nayo yaliyosalia uyatumie wewe na watoto wako..'' 
   Ndugu mpendwa katika kristo,baada ya kusoma kisa hiki cha mama huyu mjane kuna kitu hapa tutakwenda kujifunza..Zingatia hili ndugu yangu mpendwa, Mungu atabaki kuwa Mungu hata kama hajajibu jinsi wewe unavyotaka..ni lazima tuchunge mahusiano yetu na Mungu katika kila aina ya changamoto tunazopitia. Changamoto ya kifedha isikufanye ukapokea rushwa katika kazi yako..isikufanye ukapoteza uthamani wako kwa Mungu maana wewe ni wa dhamani..ooh haleluyaaa!!
Haya ni baadhi ya mambo kadhaa ambayo yatakusaidia uweze kudumu katika uhusiano na Mungu hata kama upo na changamoto za kifedha;
  • Tafuta msaada toka kwa Mungu kwanza: 
Katika hali ya kibinadamu ni kawaida kabisa kuwako hali ya kuchanganyikiwa endapo umepatwa na jambo fulani liwe tatizo au changamoto..wengi wetu huwa tunajitahidi sana kutafuta suluhisho kutoka kwa ndugu,jamaa na marafiki na wakati mwingine kukwama kabisa na wengine wasio na nguvu ya kustahimili kuishia hata kujiua..Ashukuriwe Mungu maana kuanzia leo hii hutajiua wala hutokata tamaa tena katika jina la Yesu kristo...
Mama huyu mjane ananibariki sana mana mbali na deni alokuwa nalo kumbuka alimpoteza pia mumewe..katika hali hiyo ni Mungu pekee ndo anaweza kuwa na msaada wa kweli...alichokifanya mama huyu alitafuta msaada toka kwa Mungu kwa kupitia mtumishi wake Elisha..mana alikuwa anadaiwa deni ambalo aliliacha mumewe na mdai alitaka fedha yake na kumbuka aliwataka watoto kulipia deni ile..mama huyu alitambua hana msaada mwingine zaidi ya kumkimbilia Elisha ambaye mumewe alikuwa mtumishi wake..ni kwa watumishi wa Mungu pekee ndipo tunapopata msaada. Kuna mambo mengine hayawezi kutatulika kibinadamu ni mpaka Mungu ahusishwe...

  • Kuwa mtiifu mbele za Mungu
Ndugu mpendwa katika Bwana utiifu mbele za Mungu ni kitu cha thamani sana..kutii kwako kunaweza kukawa mpenyo wa jambo lililokuwa linakutatiza muda mrefu,jawabu la maswali mengi ulokuwa ukijiuliza pasipo majibu..''Kutii kunaleta mpenyo'(Breakthrough)..Tunasoma katika kifungu chetu kile  cha 2Fal 4:2-4..Katika kifungu hiki utaona mtumishi wa Mungu Elisha alimwuliza mama yule mjane Nikufanyie nini? tena akasema, una kitu gani nyumbani? mama yule mjane ''akasema mimi mjakazi wako sina kitu nyumbani,ila chupa ya mafuta'' Baada ya hapa ndipo kutoboza kwa huyu mama kulipoanzia mana alitii maelekezo yote ya Mtumishi wa Mungu Elisha...swali la kujiuliza JE? ni mara ngapi wewe unapewa maelezo na mchungaji wako/kiongozi wako unafuata? Wengi wetu huwa tunapuuzia,wakati mwingine tunaitika bila kuyafanyia kazi..kwa jinsi hiyo huwa tunapishana na msaada kutoka kwa Mungu kwa sababu ya kutokutii kwetu..'Mungu akakupe utiifu kuanzia leo katika jina la Yesu kristo....
Baada ya kufanya kama alivyo agizwa hatimaye chupa zote zilijaa mafuta..biblia inaniambia mama huyu mjane alirudi kwa mtumishi wa Mungu Elisha kupata maelezo mengine hii inaonyesha jinsi gani mama huyu alizidi kutii mamalaka ya Kiungu..JE? ingalikuwa wewe ungerudi kwa Mtumishi wa Mungu Elisha?

  • Endeleza uhusiano na Mungu
Katika kifungu hiki 2Fal 4:7..''ndipo akaja akamwambia yule mtu wa Mungu. Naye akasema,Enenda ukayauze mafuta haya,uilipe deni yako;nayo yaliyosalia uyatumie wewe na watoto wako...
Hebu tazama mama huyu alivyokuwa na hekima ya Mungu..alikuwa na subira baaada ya vyombo kujaa,hakuwa na papara alirudi kwa Mtumishi wa Mungu Elisha kwa maelekezo zaidi..aliendeleza,alidumisha uhusiano wake na mtumishi wa Mungu..JE? ni mara ngapi wewe unafanya pasipo maelekezo ya watumishi wa Mungu? ungalikuwa ni huyu mama ungerudi kwa Elisha? Mama huyu alitambua uhusiano na Elisha ni muhimu sana kwa saa ile mana alikuwa hajui ni nini cha kufanya na yale mafuta katika vyombo vyote vile? Ndugu mpendwa kuna mamlaka ya kiungu hapa nataka uone...na mama huyu alitambua na ndo mana alirudi kwa mtumishi. Neno moja tu la kimamlaka litakupa upenyo katika maisha yako ukiwa katika mahusiano mazuri na Mungu katika hali ngumu ya kifedha kama mama huyu mjane..''Enenda ukayauze mafuta haya''.......maneno haya ya Elisha yaliambatana na mamlaka ya Kiungu ndani yake..taka yasitake mafuta yangeuzika tu kwa sababu nabii wa Bwana ametamka katika jina la Yesu kristo.....

  • Kila kitu kinaanzia nyumbani
Ndugu mpendwa hivi unafahamu baraka,ustawi,kutoboza kwako kunaanzia nyumbani? Hebu tujikumbushe tena mstari huu kuhusu mama yule mjane..''Nikufanyie nini? Niambie; una kitu gani nyumbani?...oooh haleluya...Kumbe huwezi kufanikiwa pasipokuwa na kitu nyumbani..''AKIBA'' Mama huyu mjane alikuwa na chupa ya mafuta,WEWE una nini? Mungu apate kukubariki? apate kukutoa hapo ulipo? apate kutibu ndoa yako? apate kufuta deni zako zote? Hebu tujadili mfano huu...Ukitaka kukopa fedha 'Bank' unaulizwa swali rahisi tu, Una dhamana gani? mana yake; Una akiba? Una chupa ya mafuta? Ni vizuri kuanzia hapa sasa tuanze kujiwekea chupa ya mafuta nyumbani hata siku mdeni wetu akija kuchukua chake tuwe na mafuta ya kujiuzia baadae katika jina la Yesu kristo....Kumbuka ni chupa ya mafuta pekee(AKIBA) ndiyo iliyomtoa mama yule mjane katika kufanywa wanawe watumwa...

                                                  ************AMEN***********

Friday, 20 March 2015

MAISHA NI JUKUMU LA MUDA MFUPI-2

    Ndugu wapendwa nawasalimu katika jina la Yesu kristo..Napenda kuchukua nafasi hii ya kitumishi kushiriki nanyi tena katika mwendelezo wa neno letu 'MAISHA NI JUKUMU LA MUDA MFUPI'' kadiri ya mwongozo wa Roho mtakatifu..Ni tumaini langu pia, utakuwa umeshiriki katika kumuomba Mungu akusaidie kutambua na kuyaona maisha ya hapa duniani kwa mtazamo tofauti...kumbuka katika sehemu iliyopita tuliona jinsi manabii wa zamani walivyojinyeyekesha mbele ya Mungu wetu na kumwomba awasaidie kuyaona maisha ya duniani kama ayaonavyo yeye (si yakudumu)..
Tunasoma katika biblia kitabu cha Ayubu 8:9..kwani sisi tu wa jaha tu,wala hatujui neno,kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli tu,,
   Mtumishi wa Mungu Ayubu' anazidi kutupa uhakika katika kile kitabu chake kuwa ni jinsi gani maisha ya hapa duniani yalivyo mafupi si ya kudumu tena yeye anasema kuishi kwetu hapa duniani,siku zetu ni kama kivuli tu...kwa maana hazihesabiki...Hebu tuzidi kutazama katika vitabu vingine ndani ya biblia yetu tukufu jinsi watumishi wengine mbali na Mtumishi wa Mungu Ayubu aonavyo maisha ya hapa duniani yalivyo mafupi...
   Tusome Ebr 13:4...maana hapa hatuna mji udumuo,bali twautafuta ule ujao. Katika mstari huu biblia inazidi kutuhakikishia kuwa hapa duniani si makazi ya kudumu ipo sehemu ambayo sisi ndipo tunastahili hasa kuwapo milele napo ni Mbinguni katika jina ya Yesu kristo!!!!!! Hebu tuone nini mwimba zaburi anatuambia juu ya hili tusome..Zab 39:12..Ee bwana, usikie maombi yangu,utege sikio lako niliapo,usiyanyamalie machozi yangu..kwa maana mimi ni mgeni wako,msafiri kama baba zangu wote...

    Mtunga zaburi anazidi kutufunulia kuwa mbali na kuwa wageni bali pia ni wasafiri akimaanisha tunapita hapa duniani kuna mahala tunaelekea ambapo ndipo tunastahili sisi kuwapo kama jinsi baba zake walivyokuwa wasafiri..wacha tuone tena katika kitabu cha Wakoritho kinasemaje kuhusu uhalali wetu hapa duniani je? ni wa kudumu au la...tunasoma 1Kor 7:31..Na wale wautumiao ulimwengu huu,kama hawautumii sana,kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita...tunazidi kusoma mistari mbalimbali katika vitabu mbalimbali vikituonyesha na kutuhakikishia kuwa mahala hapa si petu mambo ya hapa yote yanapita..hatupaswi kushikamana nayo mpaka tumsahau Mungu..na kumbuka Mungu ametuweka tu waangalizi mali zote na vyote vilivyomo ni vyake..tunasoma.. Zab 24:1..Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya BWANA..Dunia na wote wakaao ndani yake...hivyo yapaswa kutambua hakuna uhalali wa umiliki wowote mana sisi ni wapangaji...nyumba,fedha,magari,wanyama vyote ni vyake na sisi ni waangalizi tu..!!!!!!
Hebu tutazame tena kitabu cha 2Kor 4:18...tusiviangalie vinavyoonekana,bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele...kumbe vinavyoonekana ni vya muda tu..magari,fedha,dhahabu bali uweza wa Mungu,mamlaka yake,nguvu zake ni za milele mana hivyo huwezi kuviona katika macho haya ya damu na nyama bali ya rohoni na ndo umilele wenyewe katika jina la Yesu kristo aliye hai!!!!! na umilele huu unapatikana mbinguni ambapo ndipo makazi yetu ya milele..oooh haleluya!!!!
   Hebu tumalizie sehemu yetu ya somo kwa kutazama tena kitabu cha Efe 2:19...Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji,bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu,watu wa nyumbani mwake Mungu....ndugu msomaji wa neno hili ni katika kitabu hiki tu (Efeso) Mungu ametupa hakikisho la sisi kutokuwa wageni bali wenyeji..Kumbuka hauwezi kuwa mwenyeji kama hutafanya mapenzi yake,hutamzalia matunda,hutazifuata za kuzishika amri zake na yote haya tutayapata kwa kumsikiliza yeye aliyetumwa na yeye ambaye amefanyika dhambi ili sisi tupate patanisho na hakikisho la umilele ( yaani tusiwe wageni tena katika jina la Yesu Kristo!!!!!!!!!!

************************************AMEN*****************************

    


Tuesday, 17 March 2015

MAISHA NI JUKUMU LA MUDA MFUPI...


MAISHA NI JUKUMU LA MUDA MFUPI-1

Nawasalimu katika jina la bwana wetu Yesu kristo. Napenda kutanguliza shukrani zangu za pekee kwa Muumba wetu na kwa mpendwa mwanaye wa pekee ( Yesu kristo) kwa kunipa KIBALI hiki cha kushiriki katika neno lake takatifu.

Leo nina furaha iliyo kuu sana na ya kipekee kushiriki pamoja nanyi katika mafundisho haya mafupi ya  neno lake..Kabla sijaanza mafundisho ya neno letu la siku ya leo ambalo lina kichwa cha habari "MAISHA NI JUKUMU LA MUDA MFUPI" ningependa utambue na kukumbuka kuwa ndani ya 'NENO' ndimo kuliko na uzima..tunasoma katika kitabu cha Yoh 1:1-4..Hapo mwanzo palikuwako neno,naye neno alikuwako kwa Mungu.....

Naamini kabisa ndani ya neno hili ndimo uzima ulipo na uzima huu utakuwa nuru ndani ya maisha yako na wala giza halitakuweza kamwe. Ningependa uelewe kitu hapa ukiwa umeshiba neno au neno la Mungu limejaa ndani yako hakuna nguvu zozote za giza zitakazo kuweza..Yoh 1:5..nayo nuru itang'aa gizani,wala giza halikuiweza..ndugu mpendwa giza ni shida za kuzimu,magojwa,umasikini...neno likijaa ndani yako haya yote hayata kupata kwamwe katika jina la Yesu kristo.
.............................................................................
Tumesha elewa sasa kuwa neno ni uzima na ni nuru pia sasa naamini kabisa katika jina la Yesu kuwa somo letu la leo linakuwa uzima na nuru kwako maishani katika jina la Yesu kristo.
Somo letu la leo la MAISHA NI JUKUMU LA MUDA MFUPI,biblia imeelezea mifano mingi kupitia Wafalme na Manabii wake kuwa ni jinsi gani maisha yetu duniani yalivyo mafupi na yasiyodumu.
(mafupi-si ya umilele,yasiyodumu-ni makazi ya muda tu hivyo hatupaswi kujishikanisha nayo).
Tunasoma katika Zab 119:19..Mimi ni mgeni katika nchi,usinifiche maagizo yako. Ndugu yangu mpendwa mwimbaji zaburi anasema yeye ni mgeni katika nchi..hii ina maana kuwa hakuwa wa kudumu katika nchi ile alikuwa anapita tu ni kama alipewa hifadhi ya muda tu,ni kama alikuwa safarini kuelekea mahala fulani,ni kama safari yake haijakoma bado..ukiwa mgeni mahali una muda wa kukaa hapo na lazima uwe na kibali au ruhusa ya kuwa mahali hapo maana hapo si pako,si makazi yako unapita tu..Mfano: Umesafiri nchi ya ugeni ni lazima uwe na kibali cha kuishi pale na lazima kionyeshe ni muda gani utakuwa hapo na muda ukisha kwisha utarudi ulipo toka...ndivyo yalivyo maisha ya kiroho duniani si makazi yetu ya milele ni pa muda tu umilele wetu upo mbinguni..hivyo hatupaswi kujishikiza na vya dunia hii maana ni vya muda tu...tunasoma kitabu cha Ebr 11:13-16...hawa wote wakafa katika imani,wasijazipokea zile ahadi,bali wakaziona tokea mbali na kuzishangilia,na kukiri kwamba walikuwa wageni na wasafiri juu ya nchi......

Jambo la kuzingatia na muhimu ni kutambua kuwa kitambulisho chetu kiko katika umilele na nchi yako ni mbinguni..tunapofahamu ukweli huu tutaacha kuwa na wasiwasi wa kupata kila kitu katika dunia hii ambayo mimi na wewe ni wapangaji ndani yake.
Ningependa ushiriki nami katika kumuomba Mungu akusaidie kutambua jinsi ya muda wa kukaa hapa duniani ulivyo mfupi.....
AMEN...